Mtu huyo ambaye bado ana mioyo hiyo miwili, yupo hai na afya yake ni nzuri tangu alipofanyiwa upasuaji huo mwaka 2010.
Dk Giacomo Mugnai ambaye alihusika katika kumtibu mtu huyo anakiri kupitia barua pepe aliyotuma kwenda kwa mtandao wa msnbc.com kuwa hawajawahi kuona mgonjwa kama huyo hapo awali.
Dk Rade Vukmir, Profesa wa kitengo cha tiba ya dharura (Emergency Medicine) wa Chuo Kikuu cha America’s Temple University na msemaji wa American College of Royal Physicians anasema amewahi kushuhudia namna hiyo ya upasuaji ikifanywa katika moyo na figo huko nyuma.
Madaktari wa upasuaji kawaida huacha figo au moyo katika sehemu yake ya kawaida na kupandikiza mwingine ikiwa figo/moyo huo utakuwa kazi kubwa sana kutoa, au kama kuna matarajio ya figo/moyo huo kupona hapo siku za usoni ikiwa utasaidiwa na figo/moyo wa kupandikizwa.
Aina hii ya upasuaji (double heart transplant) ni nadra sana siku hizi kutokana na vifaa maalum ambavyo vingesaidia moyo huu wa pili wa kupandikizwa vinavyojulikana kama Ventricular Assist Devices ambavyo vilikuwa vikubwa sana na ghali miaka 20 iliyopita kuwa ni vidogo na rahisi kuvibeba katika miaka ya hivi karibuni.
Watu wanaofanyiwa upasuaji huu huishi kwa wastani wa miaka 15 baada ya kuwekea moyo wa pili lakini mtu atahitaji kufundishwa jinsi ya kuishi na moyo mwingine wa ziada, kuhudhuria hospitali mara kwa mara kuangaliwa maendeleo yake pamoja na kutumia dawa kwa muda mrefu.
Kwa habari za kawaida tembelea www.ughaibuni.com