Image

Wasiwasi kwa watoto ni jambo la kawaida na linaweza kujidhihirisha kwa njia nyingi tofauti. Ingawa hofu na wasiwasi ni sehemu ya ukuaji wa mtoto, wakati mwingine inaweza kuwa kali na kuathiri maisha yao ya kila siku. Katika makala hii, tutajadili kwa undani zaidi kuhusu wasiwasi kwa watoto, sababu zake, dalili, na njia za kukabiliana nayo.

Sababu za Wasiwasi kwa Watoto

Sababu za wasiwasi kwa watoto ni nyingi na zinaweza kuwa za kibinafsi, za mazingira, au mchanganyiko wa zote mbili. Baadhi ya sababu zinazosababisha wasiwasi kwa watoto ni pamoja na:

  • Kukabiliana Matukio hasi : Matukio kama vile kushuhudia vurugu, kutengana na wazazi, au kubadilisha shule yanaweza kusababisha wasiwasi kwa watoto.
  • Kurithi : Watoto ambao wana wazazi au ndugu walio na matatizo ya wasiwasi wana uwezekano mkubwa wa kupata matatizo haya pia.
  • Unyanyasaji au Kudhalilishwa: Watoto wanaofanyiwa unyanyasaji wa kimwili, kihisia, au kingono wana uwezekano mkubwa wa kupata wasiwasi na matatizo mengine ya afya ya akili.
  • Matatizo ya Kimwili: Matatizo ya kiafya sugu kama vile mzio (allergy) , pumu, au maumivu ya muda mrefu yanaweza kuchangia katika wasiwasi.

Dalili za Wasiwasi kwa Watoto

Dalili za wasiwasi kwa watoto zinaweza kutofautiana kulingana na umri na aina ya wasiwasi. Baadhi ya dalili za kawaida ni pamoja na:

  • Dalili za Kimwili: Maumivu ya tumbo, kichwa, au misuli; matatizo ya kulala; na mabadiliko ya hamu ya kula
  • Dalili za Kihisia: Kutokuwa na utulivu, kukasirika kwa urahisi, kulia mara kwa mara, na kujisikia kuwa na hofu kila wakati.
  • Dalili za Tabia: Kuepuka shule au shughuli za kijamii, kuzingatia sana mambo mabaya, na kuwa na shida kuzingatia.

Aina za Wasiwasi kwa Watoto

Kuna aina nyingi za wasiwasi kwa watoto, lakini baadhi ya aina za kawaida ni pamoja na:

  • Wasiwasi wa Kutengana (separation anxiety disorder): Hofu ya kutengana na wazazi au walezi.
  • Phobia Mbali mbali: Hofu kali ya vitu au hali maalum kama vile wanyama, giza, au urefu.
  • Wasiwasi wa Jamii: Hofu ya kukataliwa au kuhukumiwa (judged) na wengine katika hali za kijamii.
  • Wasiwasi wa Jumla: Wasiwasi wa mara kwa mara kuhusu mambo mbalimbali.
  • Mashambulizi ya Hofu: (panic attack) Vipindi vifupi vya hofu kali na dalili za kimwili kama vile kupumua kwa kasi na kutetemeka.

Njia za Kukabiliana na Wasiwasi kwa Watoto

Kuna njia nyingi za kukabiliana na wasiwasi kwa watoto, na matibabu bora itategemea sababu na ukali wa tatizo. Baadhi ya njia za kawaida ni pamoja na:

  • Cognitive behaviour therapy: Hii ni aina ya tiba inayomfundisha mtoto jinsi ya kutambua na kubadilisha mawazo na tabia zinazosababisha wasiwasi.
  • Dawa: Katika baadhi ya hali, dawa zinaweza kutumika pamoja na tiba ili kudhibiti dalili za wasiwasi.
  • Msaada wa Familia: Wazazi na walezi wana jukumu muhimu katika kusaidia mtoto kukabiliana na wasiwasi kwa kujenga mazingira ya usalama na upendo.
  • Mabadiliko ya Maisha: Mabadiliko katika mtindo wa maisha (lifestyle), kama vile kulala vya kutosha, kula chakula chenye afya, na kufanya mazoezi ya kawaida, yanaweza kusaidia kupunguza wasiwasi.

Hitimisho:

Ni muhimu kutambua kwamba wasiwasi kwa watoto ni tatizo linaloweza kutibiwa. Ikiwa unashuku kuwa mtoto wako ana tatizo la wasiwasi, ni muhimu kumpeleka kwa mtaalamu wa afya ya akili kwa uchunguzi na matibabu.

Homa ya kweli inasababisha wasiwasi hasa katika miezi michache ya kwanza ya maisha ya mtoto. Hii ni kwa sababu mfumo wa kinga kwa watoto huwa bado mchanga na hauna ufanisi sana katika kupambana na maambukizi kwa miezi mitatu au minne ya mwanzo baada ya mtoto kuzaliwa.

Hivyo ni muhimu kujifunza namna sahihi ipasayo kuchukua joto la mtoto wako na kuelewa nini kinaashiria homa ya kweli.

Homa kwa mtoto

Kwa kawaida madaktari husema mtoto ana homa iwapo kama joto la mwili wake litaongezeka na kufikia nyuzijoto >37.5?? (99.5F) au zaidi. Ni vizuri kujua joto la kawaida la mtoto wako kwa kuchukua vipimo mara chache wakati mtoto yupo katika hali ya kawaida ‘mzima wa afya’.

Nini husababisha homa kwa watoto?

Kuna sababu kadhaa ziletazo homa kwa watoto. Upungufu wa maji mwilini ni mojawapo ya sababu hizo. Aidha joto la watoto wachanga linaweza kuwa juu kufuatia nguo nyingi alizovaa katika mazingira ya joto kiasi. Kwa kawaida inashauriwa mtoto wako avae safu moja zaidi ya mavazi zaidi ya yale ambayo wewe mwenyewe ukivaa yanakufanya ujisikie vizuri, maana yake ni kwamba kama wewe umevaa nguo mbili juu, na ukajisikia vema, basi mtoto wako avae walau nguo tatu ili kulinda joto lake lisipungue wala kuongezeka sana.

Sababu nyingine iwezayo kuleta homa kwa watoto ni maambukizi. Mfumo wa kinga ya mwili wa mtoto unapohisi kuingiliwa na vimelea vya maradhi kama vile bacteria au virusi, hutoa taarifa kwenye ubongo ambao nao hutoa kemikali fulani zinazosababisha joto kupanda mwilini. Kupanda kwa joto huko ambako huitwa homa kunaweza kuwa na faida kadhaa katika mwilini wa mtoto zikiwemo;

  • Baadhi ya bakteria na virusi hawapendi hali ya joto la juu na hivyo basi ni rahisi zaidi kuharibiwa na mfumo wa kinga.
  • Joto la juu la mwili husaidia mwili kupambana na maambukizi.

Kucheua kwa mtoto ni hali ya mtoto kutoa chakula kupitia mdomoni muda mfupi baada ya kula/kunyonya.Kucheua kwa mtoto hupungua kadri mtoto anavyokuwa mkubwa na ni nadra sana kutokea baada ya mtoto kufikisha umri wa miezi 18.

Kucheua pia kunaweza kuashiria tatizo kubwa zaidi kwa mtoto kama ugonjwa wa Gastro-esophageal Reflux Disease (GERD), mzio (allergy) au kuziba kwa mrija wa kupitishia chakula.

Nini husababisha mtoto kucheua baada ya kula? 

  • Utafiti mpya unaonesha ya kwamba watoto wanaokunywa juisi au ambao mama zao walikunywa vitu vyenye sukari kipindi cha ujauzito wapo kwenye hatari kubwa ya kuugua ugonjwa wa Pumu
  • Wajawazito ambao walikunywa soda na vinywaji vyenye sukari (sugary beverages) wana asilimia 70 ya kuzaa watoto ambao baadae watapata ugonjwa wa Pumu

Matokeo ya utafiti kutoka Chuo Kikuu cha Harvard nchini Marekani yameonyesha ya kwamba, watoto wanaokunywa vinywaji vyenye sukari au juisi (artificial juice) na ambao mama zao walikunywa soda kipindi cha ujauzito wao wapo kwenye hatari kubwa ya kupata ugonjwa wa Pumu.

Watoto ambao waligundulika kuwa na kiwango kikubwa cha sukari aina ya fructose (ambayo hupatikana kwenye juisi au soda) kwenye milo yao kipindi cha ukuaji, walikuwa kwenye hatari ya asilimia 79 kupata ugonjwa wa Pumu ukilinganisha na watoto ambao hunywa vinywaji vyenye sukari kwa nadra au wale watoto ambao hawanywi kabisa vinywaji hivyo.

Kina mama ambao walitumia vinywaji vyenye sukari au soda kipindi cha ujauzito pia walikuwa kwenye hatari ya asilimia 70 kuzaa mtoto ambae baadae atagundulika kuwa na ugonjwa wa Pumu ikilinganishwa na kina mama ambao walitumia vinywaji vyenye sukari kwa nadra au ambao hawakutumia kabisa vinywaji hivyo kipindi cha ujauzito.

Kichwa maji au hydrocephalus (kwa lugha ya  kitaalamu) ni mkusanyiko usio wa kawaida wa maji yanayojulikana kitaalamu kama (cerebral spinal fluid) kwenye ventrikali (ventricles) au nafasi zilizo wazi (cavities) kwenye ubongo. Tafiti zinaonyesha kuenea (prevalence) kwa kichwa maji  duniani ni; kwa kila watu 100,000 basi watu 85 wana tatizo la kichwa maji na hii inatofautiana kulingana na umri.

 kwa watoto;kati ya watoto 100,000 watoto 88 wana tatizo kichwa maji.

Hali hii huweza kusababisha kuongezeka kwa shinikizo katika fuvu (increased intracranial pressure).  Hydrocephalus limetokana na lugha ya kigiriki ambalo humaanisha: Hudro - Maji , na Kephalos - Kichwa

Kwa kawaida kwa kila mtu huwa na maji yanayoitwa kitaalamu cerebral spinal fluid kifupi CSF ambayo huzunguka ndani ya ventrikali za ubongo, nje na ndani ya ubongo na kuelekea kwenye uti wa mgongo (spinal cord) ambapo hufyonzwa na kurudi kwenye damu. Kichwa maji husababishwa na uzuiwaji wa mzunguko wa CSF, au kufyonzwa kwake au uzalishwaji wa CSF kwa wingi kupita kiasi kama kwenye papilloma of choroid plexus. Ikumbukwe ya kwamba kichwa maji huweza hata kusababisha kifo.

Kuna aina mbili za kichwa maji ambazo ni

Communicating hydrocephalus (Non obstructive hydrocephalus)

Aina hii husababishwa na kutokufyonzwa kwa maji ya CSF ingawa hakuna uzuiwaji wake wa mzunguko baina ya ventrikali na nafasi iliyopo kwenye ubongo inayojulikana kama Subarachnoid space. Hii inaweza kuleta madhara kama uvujaji wa damu baina ya ventrikali au kwenye Subarachnoid space, ugonjwa wa uti wa mgongo (meningitis) nk. Aina hii ya kichwa maji nayo imegawanyika katika sehemu mbili, ambazo ni

  • Normal Pressure Hydrocephalus (NPH) – Katika aina hii ventrikali za kwenye ubongo zimeongezeka ukubwa na kuongeza pressure ya CSF.
  • Hydrocephalus ex vacuo – Katika aina hii, pia kuna kuongezeka ukubwa kwa vetrikali za ubongo na subarachnoid space kutokana na kusinyaa kwa ubongo ambapo kunaweza kusababishwa na ugonjwa wa dementia, baada ya kupata ajali ya kichwa au matatizo ya akili kama Schizophrenia.

Non communicating hydrocephalus (Obstructive hydrocephalus)

Aina hii husababishwa na uzuiwaji wa mzunguko wa CSF kwenda kwenye Subarachnoid space kutokana na uvimbe wa kwenye ventrikali.
Kwa hiyo mtu anaweza kuwa na kichwa maji kutokana na kuzaliwa nacho (congenital) au akakipata baadae maishani (acquired) baada ya kupata maradhi kwenye mfumo wa neva mwilini (CNS infections), ugonjwa wa uti wa mgongo (meningitis), uvimbe kwenye ubongo, ajali ya kichwa, kuvuja damu kwenye ventrikali nk. Kichwa maji anachopata mtu baadae maishani huwa kinaambatana na maumivu makali sana.

Kwa nini watoto wachanga wanalia?

Ni kawaida kwa watoto kulia. Hata watoto wanaozaliwa na afya njema kabisa wanaweza kulia kwa jumla ya wastani wa kati ya saa moja mpaka matatu kwa siku. Kwa vile watoto hawawezi kujifanyia chochote wao wenyewe zaidi ya kutegemea wazazi, walezi ama watu wengine wanaowazunguka katika kuwapatia chakula, joto, na faraja, kilio ni njia ya mtoto ya kuwasilisha moja ya mahitaji hayo.

Kama mzazi mpya, wakati mwingine inakuwa vigumu kutambua mtoto wako anahitaji nini anapolia. Mzazi anaweza kuwa na maswali kadhaa kichwani mwake, je, mtoto ana njaa, anasikia baridi, ana kiu, anaumwa ama amechoka? Katika siku za mwanzo, hali ya namna hii inawawia vigumu wazazi wengi, wasijue nini la kufanya. Hata hivyo, kwa kadiri siku zinavyopita mzazi mpya ataweza kutambua kuwa kilio cha mtoto wake kinamaanisha anahitaji nini kutokana na mfumo wake wa kulia.