Kwa upande wa mtoto sababu hizi ni kama zifuatazo
- Magonjwa yanayojulikana ya kuzaliwa nayo mtoto (known major fetal malformation)- Kutokukuwa kwa mfumo wa mkojo vizuri (Renal agenesis), kichwa kujaa maji (Severe hydrocephaly), kichwa kidogo (Anencephaly), matatizo katika ukuaji wa moyo (Severe cardiac anomaly), Myelomeningocele nk.
- Magonjwa ya vina saba (chromosomal abnormalities)-Down's syndrome, other trisomies, Fragile X, X-linked recessive disease kama hemophilia
- Magonjwa ya kurithi ya mfumo wa umengenyaji chakula (Inherited metabolic defect) - Duchenne muscular dystrophy, Tay-Sachs disease
- Mama kutumia dawa aina ya Warfarin,Thalidomide, Isotretoin, dawa za aina yoyote ile za saratani nk, hivyo kumuweka mtoto kwenye hatari ya kupata madhara mbalimbali.
- Mama kupewa tiba ya mionzi ya magonjwa ya saratani- dozi ya 15 rad au zaidi, kutumia tiba ya Radioactive iodine
- Mama kupata maambukizi kipindi cha ujauzito-Maambukizi ya Rubella, Cytomegalovirus, Toxoplasmosis,virusi hatari vya ugonjwa wa zika (zika virus)
Mjamzito ambaye atapata dozi ya mionzi ya kiwango cha 5 rad kwenye maeneo ya nyonga au tumbo mwanzoni mwa ujauzito wake anaweza kutoa mimba hiyo (abortion) au kuendelea kulea ujauzito wake mpaka pale atakapojifungua ikiwa yupo tayari kukabiliana na madhara ambayo mtoto wake atapata kutokana na mama kukumbana na kiwango hiki cha mionzi 1 .
Kiwango hiki cha mionzi cha 5 rad ndio kiwango cha juu cha mionzi kinachoruhusiwa kukumbana na mjamzito, lakini hii haimanishi ya kwamba mjamzito atakapokumbana na kiwango hiki cha mionzi ( 5 rad) hawezi kupata kupata mtoto aliyeathirika na mionzi, la hasha, hiki kiwango ni tahadhari ambayo mjamzito au daktari wake anapaswa ahakikishe kwamba mama huyu hafiki au kupita kiwango hiki cha (5 rad) wakati wa kufanya vipimo vyake vyote kipindi cha ujauzito.Dozi ya mionzi zaidi ya 5 rad ni hatari sana kwani mama mjamzito anaweza kuzaa mtoto mwenye saratani mbalimbali ambazo ni moja ya madhara ya mionzi wakati wa ujauzito.
Ni vyema kwa daktari kumuelimisha mama mjamzito juu ya madhara ya mionzi kwa wajawazito iwapo kuna ulazima wa kufanya vipimo venye kutoa dozi kubwa ya mionzi.
Kuomba ushauri wa kitaalamu kutoka kwa wataalamu wa fani ya jenetikali ni jambo la busara kabla ya daktari kufikia uamuzi wa kutoa mimba.Mama mjamzito mwenye tatizo la afya ambalo halina madhara makubwa sana kwake au kwa mtoto na ambalo ni mojawapo za sababu za kitabibu za kuruhusiwa kwake kutoa mimba, anaweza pia kuamua mimba yake itolewe kutokana na hisia zake juu ya ujauzito huo (wasiwasi kwamba atapata mtoto ambae ameathirika kwa madhara ya ugonjwa wake/wasiwasi kuhusu utayari wake wa kumlea na kumhudumia mtoto mwenye madhara au wasiwasi kuhusu ujauzito huo kumsumbua au hata kuhatarisha maisha yake ).
Vipimo kabla ya kutolewa mimba
- Urine for pregnancy test (UPT)-Kipimo cha mkojo cha kutambua uwepo wa ujauzito
- Kipimo cha Ultrasound-Kujua umri wa mimba, uwepo wa mimba, kufahamu iwapo viungo vya ndani vya mama ni kamilifu na havina tatizo lolote lile
- Kipimo cha X-ray-Kuangalia kama mama mjamzito ana tatizo lolote lile la moyo (kwa wale watakaochagua njia ya upasuaji) kama cardiomyopathy, moyo mkubwa (cardiomegally), tatizo la moyo linalotokana na ugonjwa wa presha
- Kupima presha (Blood Pressure monitoring) hasa kwa wale watakaochagua njia ya upasuaji
- Kipimo cha mapigo ya moyo (Pulse rate)
Kabla ya mimba kutolewa, mama mjamzito atahitaji kufanyiwa vitu vifuatavyo;
Ushauri nasaha unaolenga
- Kumpa maelezo yanayotosheleza kuhusu utoaji mimba
- Kuelimishwa jinsi ya kukabiliana na hisia zake
- Kumuondolea mama mjamzito wasiwasi
- Kumjengea ufahamu wa kuepuka mimba zisizohitajika (unplanned pregnancies)
- Kumshauri njia za uzazi wa mpango
- Kuelemishwa kuhusu njia za utoaji mimba, faida na madhara yake-Hii humsaidia mjamzito pamoja na daktari wake kushirikiana kuchagaua njia itayomfaa mama ya utoaji mimba.
Kuna aina mbili za utoaji mimba kwa mama mjamzito nazo ni
- Njia ya kutumia dawa za kutolea mimba (medical abortion)
- Njia ya upasuaji (Surgical abortion)
Ni vizuri kumfahamisha mama mjamzito ni kwa muda gani maumivu yatakuwepo baada ya kutolewa mimba pamoja na matibabu yake kwani wengi wao huwa na wasiwasi na uoga juu ya maumivu watakayopata wakati na baada ya utoaji mimba.
Mama mjamzito kusaini fomu ya kuruhusu daktari kutoa mimba yake (consent form). Hii itamsaidia mjamzito na daktari wake iwapo kutatokea tatizo lolote lile ambalo halikutarajiwa wakati au baada ya utoaji mimba. Kuhakikishiwa utunzaji wa taarifa zake za utoaji mimba. Kwamba taarifa zake hazitapewa/kutolewa kwa mtu mwingine yoyote bila ruhusa yake mama mjamzito (presumption of confidentiality). Hiki ni kipengele muhimu sana katika maadili ya udaktari.
Tuangalie njia hizi za utoaji mimba
Utoaji mimba kwa kutumia dawa za kutolea mimba (Medical abortion)
Kuna tofauti ndogo sana ya madhara na usalama wa njia hizi mbili za kutoa mimba (njia ya kutumia dawa na ya upasuaji)
Njia ya kutoa mimba kwa kutumia dawa hufanyika ikiwa mama mjamzito
- Amechagua mwenyewe njia hii
- Ana mimba yenye umri mdogo sana-Chini ya siku 49 za umri wa mimba
- Ana uzito uliopitiliza (Basal Metabolic Index kuanzia 30 na zaidi) na hana ugonjwa au tatizo lolote la moyo
- Hana tatizo lolote kwenye maumbile ya mfuko wa uzazi (uterine malformations)
- Ana uvimbe kwenye mfuko wa kizazi (fibroid)
- Aliwahi kufanyiwa upasuaji wa shingo ya kizazi (Cervical surgery)
- Anataka kuepuka njia ya upasuaji
Madhara ya utoaji mimba kwa kutumia dawa
- Kuvuja damu kutoka kwenye tupu ya mwanamke (Hemorrhage)
- Mimba kutotoka yote (Incomplete abortion)
- Maambukizi kwenye mfuko wa uzazi au kwenye mirija ya uzazi (uterine/pelvic infection)
- Kuendelea kwa uhai wa mimba na hivyo kulazimu mjamzito kutolewa mimba kwa njia ya upasuaji
- Kutotambulika/kugundulika kuwa mimba imetunga nje ya mfuko wa uzazi (ectopic pregnancy)
Kutoa mimba kwa njia ya upasuaji (Surgical abortion)
Njia hii hutumiwa iwapo mama mjamzito
- Amechagua mwenyewe
- Anapata madhara akitumia dawa za kutolea mimba mfano tatizo la mzio (allergic reactions)
- Hana muda au anaishi mbali na hospitali hivyo kushindwa kurudi hospitali kwani njia ya kutoa mimba kwa kutumia dawa inahitaji mgonjwa kurudi kwa uchunguzi zaidi ili daktari ahakikishe mimba yote imetoka na hakuna mabaki ya mimba hiyo.
Madhara ya utoaji mimba kwa upasuaji
- Kuvuja damu kutoka kwenye tupu ya mwanamke (Hemorrhage)
- Mimba kutotoka yote (Incomplete abortion)
- Maambukizi kwenye mfuko wa uzazi au kwenye mirija ya uzazi (uterine/pelvic infection)
- Kuendelea kwa uhai wa mimba na hivyo kulazimu mjamzito kutolewa mimba kwa njia ya upasuaji
- Kutotambulika/kugundulika kuwa mimba imetunga nje ya mfuko wa uzazi (ectopic pregnancy)
- Mabonge ya damu kujikusanya ndani ya mfuko wa uzazi (Hematometra)
- Kutoboka kwa mfuko wa uzazi (uterine perforation)
- Kupata madhara kwenye shingo ya kizazi (cervical laceration)