Image

Utangulizi

Neno ukimwi ni kifupisho cha maneno “Upungufu wa Kinga Mwilini”. Ugonjwa huu usabishwa na virusi ambavyo hushambulia chembe chembe za kinga na kuufanya mwili ushindwe kujilinda dhidi ya maradhi ipasavyo au hata kushindwa kupambana na maradhi yaliyoingia tayari.

Ukimwi huambukizwa kwa njia mbali mbali kama

  • kuingia damu ya mtu mwenye ukimwi kwa hasiye nao-hapo ndo kuna vitu kama kuchangia nyembe, sindano, kuwekewa damu isiyo salama n.k.
  • Kujamiiana- wadudu wa ukimwi wameonekana kuwemo kwenye majimaji ya sehemu za sili, hivyo kama kuna michubuko mtu akafanya tendo hili na mhadhilika kuna nafasi ya kuambukizwa.
  • Mama mjamzito kumuambukiza kiumbe kilichopo kwenye mfuko wakewa uzazi.

Tohara kwa wanaume ni oparesheni inayohusu kuondolewa kwa sehemu ya ngozi au ngozi yote inayofunika kichwa cha uume, na imekuwa ikifanywa na baadhi ya watu katika makabila na dini mbalimbali kwa zaidi ya maelfu ya miaka.
Kwa sasa tohara kwa wanaume imeamsha mvuto mkubwa wa kisayansi na uchunguzi kwa sababu utafiti umethibitisha kuwa wanaume waliotahiriwa wana viwango vidogo vya maambukizo ya virusi vya ukimwi (VVU) kuliko wasiotahiriwa.

Aidha ueneaji wa VVU ni mdogo kwa jumla katika jamii zinazotahiri wanaume kuliko zile ambazo wanaume hawatahiriwi. Kiasi cha asilimia 20 cha wanaume duniani kote inasemekana kuwa wametahiriwa, iwe mara baada ya kuzaliwa
au wakati wa balehe, kwa kawaida kutokana na sababu za kiutamaduni, kiafya au dini. Si nchi zote Barani Afrika zenye takwimu, kuhusu ushauri wa tohara kwa wanaume, hata hivyo kwa kawaida inakadiriwa kuwa chini ya
asilimia 20 ya wanaume kusini mwa Jangwa la Sahara wametahiriwa, kati ya asilimia 50 na 80 katika sehemu nyingi za Afrika ya Mashariki, na zaidi ya asilimia 80 au zaidi katika Bara la Afrika.


Kinachofahamika ni Nini?

Utafiti wa majaribio wa mara ya tatu Afrika Mashariki na Kusini ambao umefanywa, miaka ya hivi karibuni kupima kwa njia ya utafiti uliodhibitiwa, manufaa ya tohara kwa wanaume katika kuzuia maambukizi ya VVU. Utafiti uliofanywa katika Jimbo la Gauteng,Afrika Kusini, ulisimamishwa mapema zaidi kuliko ulivyopangwa kwa sababu matokeo yamethibitisha kuwa tohara ilikuwa kinga dhidi ya maambukizi ya VVU na wachunguzi wamependekeza kuwa utaratibu huo uendelee kwa watu zaidi ya 3,274 wanaoshiriki.

  •  Wanaume waliotahiriwa waliofanyiwa utafiti wameonekana kuwa ni asilimia 60 pungufu ya uwezekano wa kuambukizwa VVU kuliko wasiotahiriwa.
  •  Iwapo utafiti wa majaribio unaoendelea nchini Kenya na Uganda unaowahusisha wanaume 8,000 utatoa matokeo sawa na yale ya Afrika Kusini, tohara kwa wanaume itaungana na zana kama vile Kondomu za kiume na za kike kama njia kuu za kuzuia maambukizi ya VVU.
  •  Tayari msingi wa shauku umeonekana nchini Botswana na Swaziland, nchi mbili miongoni mwa nchi zilizoathiriwa sana na VVU/UKIMWI.
  •  Zaidi ya asilimia 80 ya wanaume waliofanyiwa utafiti Botswana wamesema kuwa wangependa kutahiriwa iwapo utaratibu huo ni salama na wenye gharama nafuu.
  •  Nchini Swaziland zile hospitali ambazo hazikuwa zikitahiri, sasa zimekuwa zikitahiri watu 10-15 kwa juma na zina orodha ndefu ya watu wanaosubiri huduma hiyo

 Hivyo basi kutokana na faida hizi, wanamume wanashauriwa sana kufanyiwa tohara, kwa kufanya tohara siyo tuu watakuwa wamepunguza uwezekano wa kuambukizwa VVU, bali pia watakuwa wamepunguza uwezekano wa kuwaambukiza wengine kama wao wanaishi na virusi vya ukimwi.

Ikumbukwe pia, kufanya tohara pekee hakukuondolei uwezekano wa kuambukizwa VVU, hivyo unashauriwa kuendelea kutumia njia nyingine zilizo salama za kujikinga na maambukizi ya VVU.

 

Credit: www.nacp.go.tz

VVU/Ukimwi umeenelea kuwa ni moja kati ya changamoto kubwa katika sekta ya Afya duniani haswa kwa nchi zinazoendelea. Kutokana na Takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO), inakadiriwa kuwa, kuna watu milioni 36.9 wanaishi na virusi vya ukimwi duniani kote.

Kwa siku za karibuni, kumekuwa na matokeo chanya kwenye mapambano na ugonjwa wa ukimwi, sasa hivi watu wenye virusi vya ukimwi (VVU) wanaishi maisha yenye afya njema na kwa muda mrefu kwa msaada wa dawa za kufubaza makali ya virusi vya ukimwi (antiretroviral therapy (ART)), pia matumizi sahihi ya dawa hizi husaidia kupunguza muendeleo wa uabukizaji kwa wengine.

Kazi kubwa pia imefanyika ili kuzuia na hata kumaliza kabisa maambukizi ya virusi vya ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa kujifungua.

Ingawa kuna matokeo yote hayo chanya, lakini bado kuna sehemu kubwa ya jamii bao haina uelewa juu ya ugonjwa huu, hivyo TanzMED itakuwa inakuletea dondoo chache juu ya ugonjwa huu;

1. VVU vinaweza kuambukizwa kwa njia mbalimbali kama;

  • Kuambukizwa kwa mtoto mchanga wakati akiwa tumboni, wakati wa kuzaliwa au kwa kunyonyeshwa na mama anayeishi na virusi vya ukimwi. Hivyo, kabla na baada ya kuanza kubeba ujauzito, inashauriwa kupima Afya na kuhudhuria vyema kliniki kwa ajili ya vipimo na ushauri juu na njia za kuondoa maambukizi haya.
  • Kujamiiana bila ya kinga na mtu mwenye virusi vya ukimwi
  • Kuwekewa damu yenye virusi vya ukimwi
  • Kushare vitu vyenye incha kali (sindano, viwembe, masjine za kuchorea tattoo, mikasi nk) vilivyo na virusi vya ukimwi. Watumiaji wa madawa ya kulevya wapo kwenye hatari ya kuambukizana kwakuwa wengi hutumia sindano kwa pamoja
  • Matumizi ya vifaa vya upasuaji ambavyo havijafanyiwa usafi wa kuua virusi

2. Jinsi ya kujikinga au kuzuia maambukizi ya virusi vya ukiwmi (VVU) kwa wengine

  • Hakikisha unatumia zana pindi unapofanya ngono
  • Nenda kapime na upate tiba ya magonjwa mengine ya zinaa kwani kuwa na magonjwa ya zinaa kuna uwezekano mkubwa wa kuambukizwa virusi vya ukimwi, pia kupima na kujijua mapema, kunasaiia kulinda afya yako na kuzuia kuwaambukiza wengine
  • Hakikisha damuunayowekewa imepimwa na haina virusi vya ukimwi
  • Kutahiriwa kwa wanamume kunasaidia kupunguza maambukizi (soma makala juu ya faida za tohara hapa)
  • Matumizi ya mapema na yaliyobora ya dawa za kufubama makali ya virusi vya ukimwi (ARV) husaidia kukufanya uishi na afya bora pia kupunguza maambukizi kwa wengine
  • Kuishi maisha yanayompendeza mungu kwa kuacha kuzini kabla na nje ya ndoa

Tangu kuingia kwa dawa za kuvubaza VVU (ARVs) kumeripotiwa kuwepo kwa mafanikio makubwa katika kuboresha afya za watu wanaoishi na VVU kwa kusaidia kupunguza idadi ya VVU na kuongeza idadi ya chembe nyeupe za CD4 zinazosaidia mwili kujilinda na maradhi. Lakini ARVs ni nini? Kuna makundi mangapi ya dawa hizi, zinafanyaje kazi, je zina madhara (side effects) yeyote katika mwili wa binadamu? Katika kujibu maswali haya, mwandishi wako Dk. Fabian P. Mghanga anatuletea makala ifuatayo.

Dk. Robert Kisanga aliegesha gari yake katika eneo la kuegesha magari la kituo kinachojishughulisha na huduma kwa waathirika wa ugonjwa wa UKIMWI kilichopo wilaya moja ya jiji la Dar es Salaam. Kama ilivyo kawaida ya kazi zake za kila siku, ratiba ya shughuli zake za leo inaonesha ana jukumu la kutoa mada kwa baadhi ya wateja wapya walioandikishwa kwa ajili ya kuanza matibabu ya dawa za kurefusha maisha kwa waathirika kwa ugonjwa wa Ukimwi maarufu kama ARVs.

Katika umri wake wa miaka ya mwanzo ya thelathini, Dk. Kisanga amejipatia umaarufu sana miongoni mwa wateja wake kwa sababu ya upole, ucheshi, utu na uchapakazi wake. Ni aghalabu kumkuta akiwa amekunja uso au kutoa maneno yasiyofaa na yenye maudhi kwa wale wanaomzunguka. Sifa na tabia hizi zimemfanya awe kipenzi hata kwa wafanyakazi wenzake.

Baada ya kumaliza taratibu nyingine za kikazi asubuhi ile, alielekea chumba cha mkutano, eneo ambalo lilikuwa na wateja wapya takribani thelathini wakimsubiri kwa hamu. Somo la leo lilihusu dawa za ARVs, aina, namna zinavyofanya kazi, faida na athari zake.

Ukurasa 1 ya 2