Image

Ugonjwa wa Lupus; Dalili, vipimo na matibabu yake

 

Ni moja kati ya magonjwa sugu yahusuyo mfumo wa kinga ya mwili kushambulia mwili wako na huwa na mtindo wa kuwa na kipindi cha kupata nafuu na kuwa kama umepona na kipindi cha kushambulia na kuwa hoi.

Huathiri zaidi wanawake, hadi asilimia 90 ya wagonjwa huwa wanawake. Na mara nyingi huanza kwenye umri wa uwezo wa ubebaji mimba.

Vipele ambavyo hutokea kipindi cha jua huathiri Ngozi (picha kwa hisani ya Dr. Erik Stratman, Marshfield Clinic)

 

Dalili

Ugonjwa huu huathiri karibu kila kiungo kwenye mwili

Dalili 3 kubwa ambazo hutokea ni:

  • Homa
  • Maumivu ya viungo
  • Vipele

Picha  inaonyesha vipele usoni hasa kwenye mashavu na pua kitalaamu Butterfly rash (Picha Kwa hisani ya affordablehealthinsurance.org)

Dalili nyingine ni:

  • Uchovu
  • Kupungua uzito
  • Figo kushindwa kufanya kazi vizuri
  • Dege dege
  • Maji kujaa kwenye mapafu, shinikizo la mapafu
  • Maumivu ya tumbo, kichefu chefu
  • Upungu wa damu, upungufu wa chembe chembe sahani

Vipimo:

Vipimo vya uhakika kuthibitisha ugonjwa huu ni;

  • Kipimo cha vinasaba kitaalamu double strand DNA antibodies na
  • Kingine kitaalamu Antinuclear antibody (ANA)

Vipimo vingine ni:

  • CBC- kujua wingi wa damu, na chembe chembe sahani
  • Kipimo cha damu kujua uwezo wa figo kufanya kazi (RFT)
  • Kipimo cha damu cha kujua uwezo wa ini kufanya kazi (LFT)

Matibabu:

Ugonjwa huu hauna tiba ziaidi ni kutibu dalili na kupunguza makali yake

Moja kati ya dawa ambazo hutumika ni:

  • Dawa za malaria - ambazo husaidia kupunguza makali yak inga kuushambulia mwili bila kuishusha kinga ya mwili. Dawa hizi pia huzuia na kutibu vipele ambavyo husababishwa na ugonjwa huu. Mfano wa dawa hizi ni: Hydroxychloroquine sulfate (Plaquenil)
  • Dawa za maumivu- ambazo husaidia kupunguza homa, maumivu ya kichwa na maumivu ya viungo. Mfano wa dawa hizi ni: Ibuprofen (advil, motrin)
  • Dawa za kupunguza kinga ya mwili- dawa hizi hupunguza kinga ya mwili hivyo kupunguza makali ya kushambulia mwili hivyo kupunguza makali ya ugonjwa, mfano wa dawa hizi ni: cyclophosphamide na methotrexate
  • Na kutibu kila dalili zitakazo jitokeza ipasavyo

 

 

Imesomwa mara 13831 Imehaririwa Jumatatu, 18 Novemba 2019 17:24
Dr.Mayala

Dr.Henry A Mayala ni daktari bingwa Wa Tiba ya moyo katika taasisi ya Jakaya Kikwete Cardiac Institute (JKCI), ambaye kwasasa anasomea shahada ya uzamivu (PhD) ya Tiba ya Moyo katika Chuo Kikuu cha Tongji  nchini China.

Anwani ya barua pepe hii inalindwa kutokana na spambots. JavaScript lazima iwe itawezeshwa kwa kuweza kuona.