Image

Magonjwa ya Fizi: Chanzo kingine cha kuharibu Mimba?

Baada ya kujifungua mtoto wangu wa kwanza, daktari wangu wa meno alinilalamikia kuwa situnzi vema afya yangu ya kinywa na meno. Kiukweli sikuwa nikifanya jambo lolote la ziada kuhakikisha afya yangu ya kinywa na meno iko katika hali nzuri.

Daktari wangu wa meno aliendelea kunieleza kuwa wanawake wajawazito wote na mama watarajiwa mara nyingi hupuuzia usafi wa kinywa na meno wakati wa ujauzito. Kiukweli, sikumuamini kabisa pale aliposema kuwa ujauzito husababisha mama wajawazito kubadili tabia zao za usafi wa kinywa na meno, lakini alikuwa sahihi kwa kiasi kikubwa kwa kunieleza kuwa wakati wa ujauzito vichocheo (hormones) vya mwili wa mwanamke hubadilika kwa kiwango kikubwa sana na mara nyingi huathiri afya ya fizi, hivyo ikiwa afya ya fizi ni dhaifu haiyumkini hali hii ikaathiri ukuaji wa kichanga tumboni mwa mama.

Tafiti zimethibitisha kuwa afya duni ya kinywa na meno hususani ugonjwa wa fizi unasababisha kuharibika kwa ujauzito. Tafiti iliyofanyika huko Marekani, Karolina ya Kaskazini kuangalia hali ya afya ya kinywa na meno kwa wamama watarajiwa 812, uchunguzi ulifanyika kwa kila mwanamama kwa kipindi cha majuma 26, na kisha masaa 48 baada ya kujifungua.

Watafitii walihakiki kiwango cha kuharibika mimba (chini ya majuma 28) na uzito mdogo wa kuzaliwa (chini ya 1000 gms), takwimu zilizingatia rangi ya mama (race), namba ya watoto wanaozaliwa, na jinsia ya mtoto. Asilimia 1.1 ya wamama waliokuwa na afya bora ya kinywa na meno (wamama 201) walipjifungua watoto njiti.

Kiwango hiki kiliongezeka zaid miongoni mwa wamama 566 waliokuwa na afya dhaifu ya kinywa na meno kutoka asilimia 3.5 mpaka asilimia 11.1 miongoni mwa wamama 45 waliokuwa na afya mbaya na afya mbaya zaidi ya kinywa na meno hususani magonjwa ya fizi.

Takwimu zilionyesha kuongezeka kwa kiwango cha kuzaliwa kwa watoto waliokuwa na uzito mdogo chini ya gramu 1000. Wamama wote waliokuwa na afya nzuri ya kinywa na meno walijifungua watoto wenye uzito wa zaidi ya gramu 1000.Asilimia sita (6) ya wamama wenye afya dhaifu ya kinywa na meno walijifungua watoto wenye uzito wa chini ya gramu 1000 huku asilimia 11.4 ya wamama wenye afya mbaya ama afya mbaya zaidi ya kinywa na meno walijifungua watoto wenye uzito mdogo zaidi wa chini ya gramu 1000. Tafiti zilizofanyika kwenye mataifa ya Poland, Ufaransa na Brazil yalionyesha matokeo yanayokaribiana na haya.

Matokeo ya utafiti huu yanaahusika na kuharibika kwa ujauzito ndani ya miezi sita ya awali ya mimba, kuharibika kwa mimba katika hatua za mwishoni na hata kujifungua mtoto njiti. Tatizo la magonjwa ya fizi kusababisha kuharibika kwa ujauzito na kujifungua mtoto mwenye uzito mdogo wa chini ya gramu 1000 linatokea kwa zaidi ya njia moja,kimsingi magonjwa ya kinywa na meno yanaruhusu bakteria waliomo kinywani kujipenyeza kwenye fizi na kuingia kwenye mfumo wa mzunguko wa damu, bakteria hawa wa kinywani wanapoingia kwenye mfumo wa damu husababisha kuganda kwa damu iliyopo kwenye mzunguko na hivyo kusababisha kiharusi/stroke. Bakteria hawa pia husababisha maambukizi kwenye kuta nyembamba za ndani ya moyo pamoja na valvu za moyo na moyo. Ugonjwa wa fizi usipotibiwa mapema unakomaa zaidi na kushambulia chembehai zinazoshikilia jino kwenye taya. Mara nyingine taya huathirika pia, ugonjwa hii ni hatari sana kwa ukuaji wa mimba.

Habari njema ni kuwa, ikiwa ugonjwa wa fizi utagunduliwa na kudhibitiwa mapema, hatari zote za kuharibika ujauzito ama kujifungua mtoto njiti unatoweka,

Utafiti uliofanyika Chile kuchunguza afya ya kinywa na meno miongoni mwa wamama watarajiwa wapatao 400, wenye umri kati ya miaka 18 na 35 kwa umri wa majuma ya ujauzito yasiyozidi 28. Madaktari wa meno waliwatibu wamama watarajiwa wapatao 200 mara tu baada ya uchunguzi, vile vile walitibu wamama wengine 200 mara tu baada ya kujifungua.

Matokeo yalionyesha kuwa kiwango cha kuharibika kwa ujauzito ama kujifungua kabla ya wakati na kujifungua kwa watoto wenye uzito chini ya gramu 100 walikuwa asilimia 1.8 (wamama 3/163) miongoni mwa wamama waliotibiwa mara tu baada ya uchunguzi, na asilimia 10.1 (19/188) miongoni mwa wamama ambao hawakupata tiba. Kiwango cha watoto waliozaliwa wakiwa na uzito mzito mdogo chini ya 1000 gramu na watoto njiti kilikuwa ni mara tano zaidi miongoni mwa kundi la wamama ambao hawakupata tiba.

Kuzaliwa kwa watoto njiti na watoto wenye uzito mdogo kunaongeza hatari ya kufariki kwa watoto wachanga. Bila shaka orodha ya matatizo yanayowaathiri watoto wanaozaliwa wakiwa njiti ni kubwa zaidi. Inasikitisha kuona kwamba imechukua muda mrefu sana kugundua kuwa matatizo yanayoweza kuzuilika na kutibika mapema kama magonjwa ya kinywa na meno yalivyoaathiri afya ya mama na mtoto mtarajiwa.

Tunatumai kuwa wahudumu wa afya ya mama na mtoto, mama mjamzito pamoja na madaktari wa meno watashirikiana pamoja kuzuia hatari kama hizi katika siku za usoni.

Imetafsiriwa kutoka http://ezinearticles.com

Imesomwa mara 8441 Imehaririwa Ijumaa, 09 Novemba 2018 12:12