Endapo daktari wako wa kisukari amekuhakikishi kuwa unaweza kufunga Ramadhani, haya yafuatayo ni mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa kuftari
- Pima sukari kabla ya kuftari, hii inasaidia kujua kiwango cha sukari na pia itakusaida jnsi ya kula. Kama utakuta sukari imeshuka ipo chini ya nne (4) unaweza kula chochote hata juisi ili tu kuipandisha. Na kama ipo juu ya 4,5,6,7 unaweza kumeza dawa kasha ukaftari kwa utaratibu wa kila siku.
- Ulaji wa tende wakati wa kuftari
Kwa mwenye kisukari anaruhusiwa kula tende endapo tu kiwango cha sukari kinamruhusu,kama sukari yake ipo 4 au 5 bado anaweza kula tende kwa kiasi kidogo, labda mbegu tatu au nne labda na maji au maziwa.
- Ulaji wa Matunda
- Utaratibu wa kuftari ufuate mpangilio wa kula,
Angalizo 1: Usifutari mchanganyiko wa wanga kwa wakati mmoja, mfano,muhogo,tambi, viazi,na uji, hivyo vyote ni wanga na kazi yake ni moja tu, na pia usifutari vyakula vilivyowekwa sukari,mfano, viazi vilivyowekwa sukari na maharage yaliyowekwa sukari na uji ambayo pia umewekwa sukari. Unaweza kuftari, kama mihogo kidogo,au viazi kidogo,mahagare amabayo hayana sukari, mbogamboga au kachumbali, na kikombe cha chai au maziwa badala ya uji(uji pia ni wanga)
Kama kawada ya mpangilio wa mlo kwa wenye kisukari, tunda huliwa saa moja au masaa mawili baada ya chakula, na wakati wa mfungo pia,mpangilio huu lazima ufuate, futari ni saa kumi na mbili joini, tunda liliwe saa mbili au saa tatu ya usiku, na sio matunda, liliwe tunda ya aina moja tu,kama tunda la umbo dogo,chungwa, chenza, tufaa, peasi, ni moja tu na kwa matunda yenye maumbo makubwa, papai, nanasi, embe dodo, tikiti maji, ni kipande kidogo tu.
- Pima masaa mawili baada ya kuftari au kabla hujalala
- Pima kabla ya kula daku na kabla siku hajaanza(siku mpya ya kufunga)
- Ulaji wa daku wa wenye kisukari usihusishe chakula kizito.
Angalizo 2: Makala hii sio tu kwa watu wenye Kisukari peke yao, Lah hasha. Hii ya kwa kila mmoja katika jamii yetu, baada ya mfungo kwesha wengi huongezeka uzito wa miili yao, ukifikiria kwa kina mpangilio wa ulaji kipindi cha Ramadhan hubadilika sana,kipindi hiki ulaji wa vyakula vya wanga na sukari huliwa kwa wingi na bila mpangilio.Kuna athari moja kubwa ambayo hujitokeza baada ya mfungo kuisha ambayo ni:
- Kuongezeka kwa uzito wa mwili kwa haraka ( ulaji wa vyakula vya wanga na sukar huongeza uzito kwa haraka na ni rahisi kupata maradhi ya moyo na kisukari)
kwa kumaliza, napenda kuwakumbusha kuwa kipindi cha mfungo ni kipindi takatifu kurudi kwa Allah basi ni lazima kufanya yale yote mema tuliyohusiwa na Allah na pia kuyaendeleza mara baada ya mfungo, Tumwombe Allah atufanyie wepesi katika kila jambo na aponye maradhi yanayotukabiri.
NAWATAKIA MFUNGO MWEMA WA MEZI MTUKUFU WA RAMADHANI.
Reviewed by Dr Khamis Bakari