Thomu na tangawizi iliyosagwa 2 vijiko vya chakula
Namna ya Kutayarisha na Kupika
- Tia mafuta ndani ya karai. Yakipata moto kiasi, mimina vitunguu maji na mdalasini 1 mzima kaanga. Itachukua muda kidogo. Kaanga mpaka viive viwe rangi ya hudhurungi (brown). Viepue na uweke kando.
- Ndani ya sufuria kubwa, mimina kuku, chumvi, thomu (kitunguu thomu) na tangawizi, sosi ya soya, pilipili manga, pilipili mbichi, chemsha mpaka kuku aive na maji yakauke.
- Changanya vitunguu ulivyokaanga, kabichi, pilipili, mboga, kotmiri, mchanganyiko wa mboga za barafu na weka kwa muda wa dakika tano au kumi. Tia na mafuta kidogo uliyokaangia vitunguu .
- Chemsha mchele na chumvi uive kama kawaida ya kupika wali wa kuchuja (wali wa maji). Ukishauchuja umwagie katika masala ya kuku.
- Nyunyizia mafuta kidogo uliokaangia vitunguu.
- Weka moto mdogo mpaka wali ukishaiva, uchanganye ukiwa tayari kwa kuliwa.
Dokezo
Unaweza kuupika wali huo ndani ya jiko, yaani badala ya kutia masala kwenye sufuria ukayatia katika bakuli au treya (tray) ya jiko (oven), kisha ukamwagia wali uliouchuja humo na kuupika katika moto wa nyuzi joto 400-450 kwa muda wa dakika 15-20.
Kabaabu za Kuchoma katika Vijiti
Vipimo
Nyama ya kusaga 3 lb (au kilo moja na nusu)
Thomu 1 kijiko cha chakula
Tangawizi 1 kijiko cha chakula
Chumvi Kiasi
Kotmiri 1 msongo
Bizari ya kababu ½ pakiti ya 100g
(Shan Chapplin Kabaab mix)
Namna ya Kutayarisha na Kupika
- Saga nyama pamoja na kotmiri mara mbili iwe laini kuliko ya sambusa.
- Tia kwenye bakuli na changanya na vitu vyote pamoja.
- Viringisha kwenye vijiti vya kuchomea na acha kama muda wa saa.
- Choma (bake) katika oven kwa moto wa 350?c mpaka zigeuke rangi na kuiva.
- Zikishaiva ziweke kwenye sahani tayari kwa kuliwa na saladi, chips, mikate au wali.
Dokezo
- Ni vema kuloweka vijiti vya kuchomea kwenye maji usiku nzima ili ukichoma kababu vijiti visiungue.
- Tumia bizari zako mwenyewe upendazo ikiwa huna hiyo ya Shan Chapplin Kabaab Mix.
Sharbati ya Maziwa na Shira ya Rozi
Vipimo
Shirah ya Rozi (rose syrup) ½ kikombe cha chai
Vipande vya barafu 1 Kikombe cha chai
Maziwa 4 Kikombe cha chai
Namna ya Kutayarisha
- Tia maziwa, shirah ya rozi na barafu katika jagi la kusagia (blender)
- Saga kwa muda wa dakika moja au mbili.
- Mimina sharbati kwenye gilasi ikiwa tayari.
Shukrani za Kipekee kwa tovuti ya http://www.alhidaaya.com kwa kututumia makala hii.
Kwa niaba ya timu nzima ya Tanzmed tunawatakia mfungo mwema wa mwezi wa Ramadhani. Ramadhan kareem..